Kamati ya Kitaifa ya Kupambana na Ugaidi ya Russia, imesema katika taarifa kasisi wa Kanisa la Orthodox la Russia, na maafisa wa polisi wameuwawa katika shambulizi la kigaidi.
Wizara ya Mambo ya Ndani wa Dagestan imesema kundi la watu waliokuwa na silaha lilifyatua risasi kwenye kanisa katika jiji la Derbent, lililo kwenye Bahari ya Caspian.
Washambuliaji wamekimbia na msako mkali unaendelea kuwatafuta, taarifa kutoka kwa wizara hiyo imesema. Wizara imesema wanamgambo wawili wa kundi hilo wameuwawa.
Forum