Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Julai 22, 2024 Local time: 01:07

Wanajeshi wanne wa India wauwawa


Wanajeshi wanne wa India wameuawa na wengine sita wamejeruhiwa wakati washukiwa wa uasi walipovamia gari la jeshi wakati wa doria ya kawaida katika Wilaya ya Kathua inayodhibitiwa na Wahindi, Jumatatu, kwa mujibu wa maafisa wa polisi wa India.

Katika kukabiliana na hali hiyo, polisi na vikosi vya jeshi vilisambazwa kwa haraka katika eneo hilo, kuweka uzio na kuanza msako.

Tukio hilo ambalo hakuna kundi la waasi limedai kuhusika nalo, ni la karibuni kabisa katika mfululizo wa mapigano makali.

Siku moja kabla, mapigano mawili tofauti katika wilaya ya Kulgam yalisababisha vifo vya wanajeshi wawili wa India na watu sita wanaoshukiwa kuwa wanamgambo, ripoti za polisi zinaeleza.

Mapema siku hiyo hiyo, wanamgambo walifyatua risasi kwenye kambi ya jeshi katika wilaya ya Rajouri na kumjeruhi mwanajeshi mmoja.

Kashmir inapatikana katika milima Himalaya kati ya Pakistan na India, eneo ambalo limekuwa likigombaniwa na nchi hizo tangu mwaka wa 1947.

Forum

XS
SM
MD
LG