Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 03, 2025 Local time: 00:00

Wahandishi wapendekeza kujengwa kwa zaidi ya miradi 600 ya nishati Marekani


Mtu akiendesha baiskeli karibu na Ziwa Michigan, ambako bomba la mafuta limepangwa kujengwa. Feb. 26, 2024.
Mtu akiendesha baiskeli karibu na Ziwa Michigan, ambako bomba la mafuta limepangwa kujengwa. Feb. 26, 2024.

Wahandisi wa kijeshi wa Marekani wamelenga zaidi ya miradi 600 ya nishati na miundombinu ambayo inaweza kuharakishwa chini ya mpango wa kitaifa wa Dharura ya Nishati uliotangazwa na Rias Donald Trump, kulingana na taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti yao.

Miongoni mwa miradi hiyo ni ule wa bomba la mafuta la Enbridge Line 5, chini ya ziwa Michigan, vinu kadhaa vya gesi asilia pamoja na vituo vya upelekaji gesi vilivyo pendekezwa na makampuni ya Cheniere na Venture Global.

Trump kwenye amri ya kiutendaji siku ya kwanza baada ya kuapishwa aliamuru wahandisi hao kutoa vibali vya kutumika kwa maeneo yenye maji pamoja kuchimbwa au kutengenezwa kwa njia za maji kama sehemu ya Dharura ya Kitaifa ya Nishati.

Hata hivyo kuharakishwa kwa miradi hiyo huenda kukazua mivutano ya kisheria kutokana na vibali vingi vinavyohitajika, wakati makundi ya kulinda mazingira yakionya kuwa ni ukiukwaji wa sheria za serikali kuu. Makampuni yenye kandarasi ambazo zinasubiri vibali yamekaribisha pendekezo hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG