Waziri wa ulinzi wa Marekani Pete Hegseth aliitembelea kambi ya jeshi la wanamaji ili kupata taarifa mpya kuhusu juhudi za kuwafukuza wahamiaji kwa wingi.
Ndege ya mizigo ya Marekani ikibeba wahamiaji tisa kutoka Fort Bliss huko Texas ilitua Guantanamo Bay Jumanne mchana, afisa wa wizara ya ulinzi aliiambia VOA.
Afisa wa pili alisema abiria hao wote tisa wanachukuliwa kama wahamiaji haramu hatari sana, na walipelekwa kwenye kituo hicho cha Guantanamo Bay.
Afisa wa tatu alisema ndege nyingine inayobeba wahamiaji zaidi inatarajiwa kuwasili huko leo Jumatano.
Maafisa wote hao wamezungumza na VOA kwa masharti ya kutotajwa majina kwa sababu hawaruhusiwe kuzungumzia operesheni za kuwafukuza wahamiaji.
Forum