Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 12, 2024 Local time: 23:23

Viongozi wa Marekani, Japan na Korea Kusini wasisitiza ushirikiano


Viongozi wa Korea Kusini, Japan, na Marekani walitoa taarifa ya pamoja Jumapili ya maadhimisho ya mkutano wao wa Camp David, na kuendelea kuthibitisha ahadi zao za pamoja za kukabiliana na changamoto za kikanda ofisi ya rais wa Korea Kusini imesema.

Msingi wa ushirika wa mataifa hayo matatu katika mkutano wao wa mwaka jana uliendelea kuwa mwongozo wa nchi hizo tatu wa ushirikiano, taarifa ya ofisi ya rais wa Korea Kusini, Yoon Suk Yeol imesema.

Rais wa Marekani, Joe Biden, waziri mkuu wa Japan, Fumia Kishida, na rais Yoon walikutana Agosti 18 mwaka jana, na kukubaliana kuomgeza ushirikiano wa kijeshi na uchumi na kukabiliana kwa pamoja ya ukuwaji wa nguvu ya China, na tishio la Korea Kusini.

Vyombo vya habari vya Korea Kusini vimesema kwamba viongozi hao wanatarajiwa kukutana tena mwaka huu vikinukuu vyanzo ambavyo havikutajwa.

Forum

XS
SM
MD
LG