Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 07, 2024 Local time: 05:23

Viongozi wa Iran watakiwa kuwajibishwa kwa manyanyaso ya miaka ya 1980


Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa, Jumatatu ametoa mwito wa uchunguzi wa kimataifa kuhusu uhalifu wa ukatili ikiwa pamoja na mauaji ya halaiki, yaliyofanyika Iran dhidi ya wanaoamini dini ndogo na kuondolewa kwa wapinzani katika miaka ya 1980.

Javaid Rehman, mtaalamu huru na maalum wa Umoja wa Mataifa wa hali ya haki Iran, amesema lazime kuwe na uwajibikaji kwa ukiukwaji huo mkubwa wa haki za binadamu, bila kujali lini ulifanyika.

“Utawala wa Iran na viongozi wake hawapaswi kuruhusiwa kuepuka matokeo ya uhalifu wao dhidi ya ubinadamu na mauaji ya kimbari,” aliongeza.

Mtaalamu huyo ambaye mamlaka yake yatakamilika Julai 31, amesema katika taarifa yake kwamba uhalifu wa ukatili wa mauaji ya kiholela nje ya mahakama ya 1981 na 1982 pamoja na 1988 yalitokana na uhalifu dhidi ya ubinadamu wa mauaji na yale ya kimbari.

Forum

XS
SM
MD
LG