Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 21, 2024 Local time: 10:49

Vifaa vya mashirika ya kutoa misaada Haiti vyaibiwa


(MKATABA) Ghasia nchini Haiti.
(MKATABA) Ghasia nchini Haiti.

Mashirika  kadhaa ya serikali na yale ya kutoa  misaada nchini Haiti yameripoti kuwa vifaa vyao,  pamoja na misaada imeporwa, huku nchi hiyo ikiingia kwenye wimbi jingine la ghasia za magenge.

Makundi ya wahalifu yamevamia Haiti katika wiki za hivi karibuni kushambulia taasisi muhimu na kufunga uwanja mkuu wa ndege wa kimataifa. Machafuko hayo yamewasukuma raia wengi wa Haiti kwenye ukingo wa njaa, na kuwaacha wengi zaidi katika hali ya kukata tamaa.

UNICEF ilisema kuwa kontena la usafirishaji lililojaa vifaa muhimu vya msaada limeporwa huku serikali ya Guatemala ikisema kuwa kituo cha ubalozi pia kiliibiwa.

Marekani ilikuwa imepeleka kwa ndege vikosi vya kijeshi ili kuimarisha usalama katika Ubalozi wake, na pia kufanya kile kilichoonekana kama kukanusha uvumi kwamba maafisa wakuu wa serikali ya Marekani wanaweza kuondoka nchini humo.

Forum

XS
SM
MD
LG