Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Septemba 18, 2024 Local time: 03:26

UN imelaani ongezeko la vifo katika makundi ya kutoa misaada ya kibinadamu


Mfano wa misaada ya kibinadamu inayotolewa na makundi ya kutoma misaa ya kibinadamu kimataifa. Feb. 17, 2023.
Mfano wa misaada ya kibinadamu inayotolewa na makundi ya kutoma misaa ya kibinadamu kimataifa. Feb. 17, 2023.

Mwaka 2023 ulikuwa mbaya zaidi kwa makundi yanayotoa misaada ya kibinadamu duniani ambapo rekodi ya vifo imefikia 280

Umoja wa Mataifa umelaani kiwango cha ghasia kisichokubalika na kuwa cha kawaida dhidi ya wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu, rekodi imefikia 280 ambao waliuawa duniani kote mwaka 2023.

Imeonya kuwa vita vya Israel na Hamas huko Gaza vinaweza kuchochea idadi kubwa zaidi ya vifo kama hivyo mwaka huu. “Kuhalalisha vurugu dhidi ya wafanyakazi wa misaada na ukosefu wa uwajibikaji ni jambo lisilokubalika, lisilojali na lenye madhara makubwa kwa shughuli za misaada kila mahali,” Joyce Msuya, kaimu mkurugenzi wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya uratibu wa masuala ya kibinadamu (OCHA), alisema katika taarifa yake ya siku ya kimataifa ya kibinadamu.

"huku wafanyakazi 280 wa misaada waliuawa katika nchi 33 mwaka jana, mwaka 2023 ulikuwa mwaka mbaya zaidi kwa makundi yanayotoa misaada ya kibinadamu duniani,” ongezeko la asilimia 137 zaidi ya mwaka 2022, wakati wafanyakazi wa misaada 118 walikufa, OCHA ilisema katika taarifa.

Forum

XS
SM
MD
LG