Timu ya waangalizi wa vikwazo ya Umoja wa Mataifa ilitoa tathmini hiyo Jumatano usiku wakati kukiwa na ongezeko kubwa la mashambulizi ya kigaidi yanayoongozwa na TTP dhidi ya vikosi vya usalama vya Pakistani na raia, na kuua mamia yao katika wiki za hivi karibuni.
Ripoti imesema TTP inaendelea kufanyakazi kwa kiwango kikubwa Afghanistan kwa operesheni za kigaidi Pakistan kutoka huko, mara nyingi kwa kutumia Waafghani.
Ilibainisha kuwa kundi lililo tangazwa kimataifa kuwa la kigaidi na kujulikana pia kama Taliban wa Pakistani, linaendesha shughuli zake nchini Afghanistan likiwa na wastani wa wapiganaji kati ya 6,000 na 6,500.
Forum