Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 14, 2025 Local time: 06:30

Ukraine yapata zaidi ya dola bilioni 1 za msaada  mpya wa kijeshi kutoka Ubelgiji


Waziri Mkuu wa Ubelgiji Alexander De Croo, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na Waziri wa Ulinzi wa Ubelgiji Ludivine Dedonder wakisikiliza walipokutana na marubani wa Ubelgiji wa F-16, wakufunzi na wafanyakazi wa kiufundi wakati wa ziara ya ukaguzi
Waziri Mkuu wa Ubelgiji Alexander De Croo, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na Waziri wa Ulinzi wa Ubelgiji Ludivine Dedonder wakisikiliza walipokutana na marubani wa Ubelgiji wa F-16, wakufunzi na wafanyakazi wa kiufundi wakati wa ziara ya ukaguzi

Ukraine ilipata zaidi ya dola bilioni 1 za msaada  mpya wa kijeshi kutoka Ubelgiji katika makubaliano leo  Jumanne ambayo yanajumuisha ndege 30 za kivita aina ya F-16.

Makubaliano hayo yalikuja wakati Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy alipoitembelea Brussels katika safari ambayo pia inajumuisha kwenda Uhispania na Ureno kutafuta msaada mpya wa kupambana na uvamizi wa Russia ulioanza mapema mwaka 2022.

Makubaliano hayo yanahakikisha msaada wa usalama wa Ubelgiji kwa wakati unaofaa, magari ya kisasa ya kivita, vifaa vya kukidhi mahitaji ya jeshi la anga na ulinzi wa anga wa Ukraine, usalama wa majini, kuondoa mabomu ya kutegwa ardhini, ushiriki katika muungano wa silaha za kivita, na mafunzo ya kijeshi, Zelenskyy alisema kwenye mtandao wa X.

Kiongozi huyo wa Ukraine alisema makubaliano hayo ya miaka 10 pia yanajumuisha kushirikiana na Ubelgiji katika masuala ya kijasusi, usalama wa mtandao, kukabiliana na taarifa potofu na sekta ya ulinzi.

Forum

XS
SM
MD
LG