Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 19, 2024 Local time: 11:54

Ukraine yaharibu madaraja matatu ya Russia


Vikosi vya Ukraine, vimeharibu madaraja yote matatu ya Mto Seym magharibi mwa Russia, kwa mujibu wa vyanzo vya Russia, wakati uvamizi wa Kyiv ukiingia wiki yake ya tatu Jumanne.

Kuvamia kwa Kyiv katika eneo la Kursk la Russia, kunabadilisha mwelekeo wa vita na kuongeza ari kati ya wakazi waliochoshwa na vita kwa Ukraine, ingawa hatma ya uvamizi huo ambao ni shambulizi la kwanza dhidi ya Russia, toka vita vya pili vya dunia haijulikani.

Licha ya Ukraine kujipongeza kwa mafanikio yake ndani ya Russia, msukumo wa Russia, mashariki mwa Ukraine uko tayari kuchukuwa sehemu nyingine muhimu ya mji wa Pokrovsk.

Mashambulizi ya Ukraine kwenye madaraja matatu juu ya Mto Seym, yanaweza kuzuia vikosi vya Russia kuvuka mto huo, Ukraine kusonga mbele kwenye mpaka wake.

Tayari wanaonekana kupunguza kasi ya majibu ya Russia kwaa uvamizi wa Kursk, ambao Ukraine iliuanzisha Agosti 6.

Forum

XS
SM
MD
LG