Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 01:09

Uhusiano wa Marekani na Russia


Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rubio. Februari 19, 2025
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rubio. Februari 19, 2025

Wanadiplomasia wa Marekani na Russia wamekutana leo alhamisi Istanbul kwa mazungumzo kuhusu utendakazi wa balozi zao mjini Moscow na Washington.

Mkutano huo ni wa hivi punde katika msururu wa mikutano kati ya pande hizo mbili, ikiwemo mazungumzo ya simu mapema mwezi huu kati ya rais wa Marekani Donald Trump na mwenzake wa Russia Vladimir Putin.

Wiki iliyopita, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio na mwenzake wa Russia Sergey Lavrov walikutana na miongoni mwa maswala wanayojadiliana ni namna ya kurejesha uhusiano mwema kati ya Marekani na Russia

Baada ya mazungumzo hayo, Wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema kwamba mazungumzo ya Riyadh yalifikia makubaliano ya kuunda mbinu ya kushauriana ili kushughulikia maswala yanayovuruga uhusiano kati ya nchi hizo mbili, kwa lengo la kuboresha uhusiano wa kidiplomasia.

Uhusiano kati ya Marekani na Russia umekuwa mbaya kwa muda wa muongo uliopita, pande zote zikifukuza wanadiplomasia kutoka upande mwingine.

Forum

XS
SM
MD
LG