Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Septemba 29, 2024 Local time: 02:30

Uhispania imekuwa ya kwanza Ulaya kuiomba mahakama ya Umoja wa Mataifa kujiunga katika kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel


Waziri wa mambo ya nje wa Spain s Jose Manuel Albares akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya wizara hiyo mjini Madrid Juni 6, 2024.
Waziri wa mambo ya nje wa Spain s Jose Manuel Albares akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya wizara hiyo mjini Madrid Juni 6, 2024.

Uhispania imekuwa nchi ya kwanza ya Ulaya kuiomba mahakama ya Umoja wa Mataifa kujiunga katika kesi ya Afrika Kusini inayoishutumu Israel kwa mauaji ya kimbari huko Gaza.

Uhispania imekuwa nchi ya kwanza ya Ulaya kuiomba mahakama ya Umoja wa Mataifa kujiunga katika kesi ya Afrika Kusini inayoishutumu Israel kwa mauaji ya kimbari huko Gaza.

Afrika Kusini iliwasilisha kesi yake katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki mwishoni mwa mwaka jana. Ilidai kuwa Israel ilikuwa inakiuka mkataba wa mauaji ya halaiki katika mashambulizi yake ya kijeshi ambayo yameharibu maeneo makubwa ya Gaza.

Mahakama hiyo imeiamuru Israel kusitisha mara moja mashambulizi yake ya kijeshi katika mji wa kusini mwa Gaza wa Rafah lakini ikaacha kuamuru sitisho la mapigano katika eneo hilo. Israel haijatii na haonyeshi dalili ya kufanya hivyo.

Forum

XS
SM
MD
LG