Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Oktoba 23, 2024 Local time: 06:33

Ufaransa inatuma vikosi vya kijeshi kusambaza maji katika kisiwa cha Mayotte


Watu wakipanga foleni ili kupata maji huko Tsoundzou, katika kisiwa cha Mayotte Jumamosi Feb.6, 2021.AP
Watu wakipanga foleni ili kupata maji huko Tsoundzou, katika kisiwa cha Mayotte Jumamosi Feb.6, 2021.AP

 Vikosi vya jeshi la Ufaransa vya nje na jeshi la wanamaji la Ufaransa walio katika eneo hilo watafanya kazi na serikali za mitaa kuhakikisha usambazaji wa maji kwa wakaazi wa eneo hilo, Wizara ya Ulinzi ilisema katika taarifa siku ya Alhamisi.

Ufaransa inatuma vikosi vya kijeshi kusambaza maji katika eneo la Bahari ya Hindi la Ufaransa la kisiwa cha Mayotte, ambacho kinakabiliwa na shida ya maji ambayo haijawahi kushuhudiwa kutokana na ukame mkubwa zaidi katika kisiwa hicho katika miongo kadhaa.

Vikosi vya jeshi la Ufaransa vya nje na jeshi la wanamaji la Ufaransa walio katika eneo hilo watafanya kazi na serikali za mitaa kuhakikisha usambazaji wa maji kwa wakaazi wa eneo hilo, Wizara ya Ulinzi ilisema katika taarifa siku ya Alhamisi.

Mamlaka imeamuru kukatwa maji kwa siku mbili kati ya tatu huko Mayotte, eneo la kaskazini magharibi mwa Madagascar ambalo ni sehemu maskini zaidi ya Ufaransa. Matatizo ya maji yanakuja juu ya mvutano wa uhamiaji kutoka kwa watu wanaowasili kutoka nchi jirani ya Comoro.

Forum

XS
SM
MD
LG