Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 05:17

Trump asema ushuru mpya kwenye bidhaa za Mexico na Canada kuanza kutekelezwa wiki ijayo


Rais Donald Trump akisaini amri ya kiutendaji kuhusu tozo sawa ya ushuru kwa bidhaa kutoka nchi washirika wa kibiashara wa Marekani, Februari 13, 2025. Picha ya AFP
Rais Donald Trump akisaini amri ya kiutendaji kuhusu tozo sawa ya ushuru kwa bidhaa kutoka nchi washirika wa kibiashara wa Marekani, Februari 13, 2025. Picha ya AFP

Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba ataweka ushuru wa asilimia 25 kwenye bidhaa kutoka Canada na Mexico wiki ijayo kama alivyopanga hapo awali, akidai kuwa nchi hizo mbili, Jirani za Mrekani, bado hazifanyi vya kutosha kuzuia dawa za kulevya kuingia Marekani.

Aidha, Trump alisema kwenye mtandao wake wa kijamii Truth Social kwamba ataiwekea China ushuru mwingine wa asilimia 10 Jumanne ijayo kwenye bidhaa zake inazouza Marekani, kuongeza kwenye ushuru wa asilimia 10 alioweka mapema mwezi huu.

China iliweka kwa haraka ushuru sawa na ule wa kwanza wa Trump kwenye bidhaa za Marekani.

“Dawa za kulevya bado zinaingia kwa wingi nchi mwetu kutoka Mexico na Canada kwa viwango vya juu na visivyokubalika,” Trump alisema.

“Kiwango kikubwa cha dawa hizi, nyingi zikiwa aina ya Fentanyl, zinatengenezwa China na kusafirishwa na nchi hiyo.”

Trump alitangaza kwanza ushuru kwenye bidhaa za Canada na Mexico, washirika wawili wa karibu wa Marekani na washirika wa kibiashara, mapema mwezi huu.

Forum

XS
SM
MD
LG