Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Septemba 13, 2024 Local time: 04:08

Taliban waendelea kukandamiza vyombo vya habari, yanasema mashirika ya kutetea haki za wanahabari


Msemaji wa serikali ya Taliban Zabihullah Mujahid
Msemaji wa serikali ya Taliban Zabihullah Mujahid

Mashirika ya kutetea haki za waandishi wa habari yanasema kusimamishwa kwa leseni za utangazaji, kukamatwa kwa waandishi wa habari na kufungwa kwa vyombo vya habari nchini Afghanistan, inaonyesha kuwa Taliban wanaendelea kukandamiza vyombo vya habari.

Katika wiki za hivi karibuni, Mamlaka inayodhibiti mawasiliano ya serikali ya Taliban, au ATRA, ilisimamisha leseni 17 za utangazaji zilizopewa vyombo vya habari katika jimbo la mashariki la Nangarhar.

Kituo cha radio cha kibinafsi cha Kawoon Ghag katika jimbo la Laghman pia kimefungwa, kulingana na mashirika yanayofuatilia uhuru wa vyombo vya habari.

“Miaka mitatu baada ya Kabul kutekwa, Taliban wanaendelea kuwakandamiza wanahabari na vyombo vya habari vinavyoendelea kufanya kazi nchini Afghanistan,” Beh Lih Yi, mtaratibu wa program katika shirika la Committee to protect Journalists kanda ya Asia, aliiambia VOA.

Alisema kupitia barua pepe kwamba“Mwezi Julai pekee, waandishi wa habari wawili, Sayed Rahim Saeedi na Mohammad Ibrahim Mohtaj, walikamatwa na maafisa wa ujasusi wa Taliban na polisi wa maadili.

Forum

XS
SM
MD
LG