Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 20:20

Taliban hawataki ICC kuingilia maswala ya Afghanistan


Wapiganaji wa Taliban wakiwa mjini Kabul, Aug. 31, 2022.
Wapiganaji wa Taliban wakiwa mjini Kabul, Aug. 31, 2022.

Viongozi wa Taliban wenye msimamo mkali nchini Afghanistan, wamekataa mamlaka ya mahakama ya uhalifu wa kimataifa ICC nchini humo, na kutangaza hatua ya waliokuwa viongozi wa nchi hiyo kuingiza Afghanistan katika makubaliano ya ICC mwaka 2003, kuwa kinyume cha sheria.

Hatua hiyo inafuatia tangazo la mwendesha mkuu wa mashtaka wa ICC, mwezi uliopita, la kutaka kiongozi wa juu zaidi wa Taliban Hibatullah Akhundzada na washirika wake wa karibu kukamatwa.

ICC inawashutumu kwa kuwajibika na uhalifu wa kuwatesa wanawake na wasichana wa Afghanistan.

Taliban walichukua uongozi wa Afghanistan mnamo Agosti 2021, kutoka kwa serikali iliyokuwa ikitambuliwa kimataifa ya Kabul, iliyoanguka baada ya Marekani kuondoa wanajeshi wake nchini humo baada kulinda amani kwa muda wa miongo miwili.

Taliban, wanaongoza Afghanstan kwa kutumia sheria kali za Kiislamu, na kuwawekea vizuizi vikali wanawake ikiwemo kukandamiza uhuru wa kujieleza, kuwazuia kusoma shuleni na kushiriki shughuli za uma katika jamii.

Hakuna nchi imetambua utawala wa Taliban kutokana na namna wamewakandamiza wanawake na Watoto wasichana.

Forum

XS
SM
MD
LG