Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 12, 2024 Local time: 00:13

Shirika la ulinzi wa kiraia la Gaza lasema shambulizi la Israeli limeuwa watu 15 kutoka familia moja  ya Kipalestina


Moshi ukifuka kufuatia shambulio la anga la Israel huko Rafah, Oktoba 30 2023. Picha na SAID KHATIB / AFP.
Moshi ukifuka kufuatia shambulio la anga la Israel huko Rafah, Oktoba 30 2023. Picha na SAID KHATIB / AFP.

Shirika la ulinzi wa kiraia la Gaza limesema shambulizi la anga la Israel alfajiri ya Jumamosi liliuwa watu 15 kutoka familia moja  ya Kipalestina, wakiwemo watoto tisa na wanawake watatu.

Shambulizi hilo lilipiga nyumba ya familia ya Ajlah katika kitongoji cha Al-Zawaida katikati mwa Gaza, msemaji wa ulinzi wa raia Mahmud Bassal aliambia AFP. Jeshi la Israel halikutoa maoni yake mara moja.

"Idadi ya waliofariki kutokana na shambulio la Israeli kwenye nyumba ya familia ya Ajlah na ghala lao huko Al-Zawaida imefikia 15," Bassal alisema.

Bassal alitoa orodha ya waliouawa, wakiwemo watoto tisa na wanawake watatu.

Shahidi mmoja alisema shambulio hilo lilifanyika muda mfupi baada ya saa sita usiku.

Forum

XS
SM
MD
LG