Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 12, 2025 Local time: 22:45

Serikali ya mpito Syria


Mwanamme akikagua gereza la Saydnaya, kaskazini mwa Damascus Dec 16 2024
Mwanamme akikagua gereza la Saydnaya, kaskazini mwa Damascus Dec 16 2024

Kiongozi wa muungano wa kitaifa wa Syria Hadi al-Bahra, waliomuondoa rais Bashar Al-Assad amesema kwamba serikali ya mpito ya Syria inastahili kuhusisha kila chama cha Syria na wala sio kuwa na ubaguzi.

Akizungumza katika kikao na waandishi wa habari mjini Istanbul, Uturuki, Bahra amesema kwamba waakilishi wa muungano wa kitaifa wa Syria hawajakutana na kiongozi wa waasi wa Syria Ahmed al-Sharaa, lakini wamewasiliana na serikali ya mpito na washirika walio karibu naye.

Waasi wa Syria walidhibithi mji mkuu wa Damascus Desemba 8 na kumlazimu Assad kutoroka nchini baada ya miaka 13 ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, na kumaliza utawala wa kifamilia wa miongo kadhaa.

Mapinduzi ya Syria yamesababisha hali ya wasiwasi, iwapo kutakuwa na ubadilishanaji wa Madaraka kwa njia ya utulivu.

Forum

XS
SM
MD
LG