Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Septemba 06, 2024 Local time: 15:14

Serikali ya Kenya yaongeza wito wake kwa wiki kadhaa za maandamano kusitishwa


Waandamanaji waliitikia wakati wa maandamano kupinga muswaada wa fedha wa Kenya wa 2024/2025, Nairobi, Kenya, Juni 20, 2024. REUTERS/Monica Mwangi
Waandamanaji waliitikia wakati wa maandamano kupinga muswaada wa fedha wa Kenya wa 2024/2025, Nairobi, Kenya, Juni 20, 2024. REUTERS/Monica Mwangi

Serikali ya Kenya siku ya Alhamisi iliongeza wito wake kwa wiki kadhaa za maandamano kusitishwa huku polisi wakipiga marufuku maandamano katikati mwa mji mkuu Nairobi, wakisema kuwa yameingiliwa na magenge ya wahalifu.

Baadhi ya wanaharakati waliwataka watu kukusanyika siku ya Alhamisi wakiwa na vifaa vya kupigia kambi ili kukaa katika bustani ya Uhuru iliyo karibu na katikati mwa jiji, huku kukiwa na wingi wa polisi kote Nairobi.

Watu wasiopungua 50 wameuawa katika maandamano yaliyoongozwa na vijana kupinga mapendekezo ya nyongeza ya kodi yaliyozuka kote nchini Kenya mwezi mmoja uliopita na yameendelea hata baada ya Rais William Ruto kuondoa muswaada wa sheria hiyo na kuwafuta kazi takriban baraza lake lote la mawaziri.

Wanasema wanataka Ruto ajiuzulu na wanataka mageuzi yafanyike ili kuondoa ufisadi na kushughulikia utawala mbovu.

Forum

XS
SM
MD
LG