Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Oktoba 07, 2024 Local time: 06:05

Rais wa Ufaransa akataa kujiuzulu kwa Waziri Mkuu katika serikali yake


Waziri Mkuu wa Ufaransa, Gabriel Attal ambaye Rais Macron amekataa barua ya kujiuzulu kwake.
Waziri Mkuu wa Ufaransa, Gabriel Attal ambaye Rais Macron amekataa barua ya kujiuzulu kwake.

Wapiga kura wa Ufaransa waliligawa bunge katika mrengo wa kushoto, katikati na kulia

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekataa kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, akimuomba hii leo Jumatatu kuendelea kuwepo kwa muda kama kiongozi wa serikali baada ya matokeo ya uchaguzi yenye vurugu kuiacha serikali katika hali ya wasiwasi.

Wapiga kura wa Ufaransa waliligawa bunge katika mrengo wa kushoto, katikati na kulia, na hakuna kundi lolote litakalokaribia wingi wa kura zinazohitajika kuunda serikali. Matokeo kutoka kura ya Jumapili yameongeza hatari ya kupunguza kasi ya uchumi wa pili kwa ukubwa katika Umoja wa Ulaya.

Macron alisema uamuzi wake wa kuitisha uchaguzi mdogo utaipa Ufaransa “muda wa ufafanuzi”, lakini matokeo yalionyesha kinyume, chini ya wiki tatu kabla ya kuanza kwa michuano ya Paris Olimpiki, wakati nchi hiyo itakuwa katika jukwaa la kimataifa.

Forum

XS
SM
MD
LG