Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Agosti 13, 2024 Local time: 05:53

Raia wa Rwanda kupiga kura Jumatatu kumchagua rais wa nchi hiyo


 Wafuasi wa Rais wa Rwanda Paul Kagame wakicheza wakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi huko Kigali, Rwanda, Ijumaa, Julai 12, 2024.
Wafuasi wa Rais wa Rwanda Paul Kagame wakicheza wakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi huko Kigali, Rwanda, Ijumaa, Julai 12, 2024.

Raia wa Rwanda wanapiga kura Jumatatu katika uchaguzi ambao bila shaka utarefusha muda mrefu wa utawala wa Rais Paul Kagame, ambaye anagombea bila kupingwa baada ya miongo mitatu madarakani katika taifa hilo la Afrika Mashariki.

Kagame amekutana na umati wa wafuasi waliompokea kwa furaha kwenye mikutano ya kampeni ambayo inadhihirisha kutoepukika kwa ushindi wake anapowania muhula wa nne kama rais. Wakati wapinzani wake Frank Habineza wa Democratic Green Party of Rwanda na mgombea huru Philippe Mpayimana wamepata taabu kuvuta umati kwenye hafla zao.

Kagame alikabiliana na wapinzani hao hao mwaka 2017, alipopata karibu asilimia 99 ya kura. Wafuatiliaji wanasema matokeo kama hayo yanatarajiwa katika nchi ambayo upinzani mkubwa dhidi ya Kagame haujakuwepo kwa muda mrefu.

Kagame mwenye umri wa miaka 66, alichukua mamlaka kama kiongozi wa waasi waliochukua udhibiti wa serikali ya Rwanda na kumaliza mauaji ya kimbari mwaka 1994. Kagame alikuwa makamu wa rais wa Rwanda na kiongozi mkuu kutoka 1994 hadi 2000, alipokuwa rais kwa mara ya kwanza. Tangu wakati huo ametawala nchi hiyo ya Afrika Mashariki kama mtawala asiyevumilia upinzani wa kisiasa.

Forum

XS
SM
MD
LG