Mkutano huo unachukuliwa na Moscow na Beijing kuwa muhimu sana katika kukabiliana na ushawishi wa Marekani na washirika wake.
Putin na mwenzake wa China, wamepanua ushirikiano wa Shanghai, ulioanzishwa na Russia, China na nchi zilizo katikati mwa Asia mwaka 2001, na kujumulisha India, Iran na Pakistan kama mkakati wa kukabiliana na ushawishi wa nchi za magharibi.
Putin atafanya mikutano na viongozi wenzake pembezoni mwa mkutano huo unaofanyika Kazakh, Astana.
Atakutana na Xi, Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki na viongozi wa Azerbaijan, Mongolia na Pakistan.
Forum