Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Agosti 12, 2024 Local time: 19:20

Pakistan imepokea mkopo muhimu kutoka IMF


Waziri wa fedha wa Pakistan Muhammad Aurangzeb katika mahojiano na shirika la habari la AFP. April 15, 2024.
Waziri wa fedha wa Pakistan Muhammad Aurangzeb katika mahojiano na shirika la habari la AFP. April 15, 2024.

Pakistan imesema kwamba mkopo mpya wa mabilioni ya dola ambao imepokea kutoka kwa shirika la fedha la kimataifa IMF, utasaidia nchi hiyo kuimarisha uchumi wake ambao una upungufu mkubwa wa fedha.

Taarifa hiyo imetolewa saa chache baada ya IMF kutangaza makubaliano ya mwanzo na Islamanad kutoa mkopo wa dola bilioni 7 wa muda wa miezi 37.

Mkopo huo unasubiri kuidhinishwa na bodi ya utendaji ya IMF na kujpatikana kwa mkopo huo ni muhimu kwa Pakistan kwa ajili ya mipango yake ya maendeleo.

Hakuna tarehe kamili ambayo bodi ya IMF itaidhinisha mkopo huo, lakini ni hatua ya mchakato tu kabla ya pesa kutolewa.

Waziri mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif ametangaza taarifa hiyo leo Jumamosi wakati wa kikao na timu yake ya wataalam wa fedha na kuwasifu kwa kufanya mazungumzo yaliyopelekea kupatikana kwa mkopo huo.

Forum

XS
SM
MD
LG