Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Februari 19, 2025 Local time: 14:50

Ndege ya abiria yagongana na helikopta ya kijeshi kwenye uwanja wa Reagan National


Boti yaonekana karibu na eneo la tukio ya ajali ya ndege karibu na uwanja wa ndege wa Reagan Washington National Airport, Januari 30, 2025. Picha ya AP
Boti yaonekana karibu na eneo la tukio ya ajali ya ndege karibu na uwanja wa ndege wa Reagan Washington National Airport, Januari 30, 2025. Picha ya AP

Ndege ya abiria iligongana na helikopta ya kijeshi ya Marekani Jumatano usiku wakati ilipokuwa inakaribia kutua kwenye uwanja wa ndege wa Washington DC Reagan National, Mamlaka ya usafiri wa anga FAA ilisema.

Taarifa ya FAA ilisema ndege ya shirika la American Airlines ilikuwa ikisafiri kutoka Witchita, Kansas, na ilikuwa inakaribia njia yake ya kutua ilipogongana na helikopta aina ya Sikorsky H-60 nyakati za saa tatu usiku.

Hakuna taarifa kuhusu maafa iliyotolewa mara moja.

Maafisa walisema wanajeshi watatu wa Marekani walikuwa ndani ya helikopta hiyo. American Airlines ilisema katika taarifa kwamba abiria 60 na wahudumu wanne walikuwa ndani ya ndege hiyo.

“Tunathibitisha kwamba ndege iliyohusika katika ajali ya usiku ilikuwa helikopta ya kijeshi aina ya UH-60 nje ya Belvoir, Virginia,” jeshi lilisema katika taarifa.

“Tunashirikiana na maafisa wa eneo hilo na tutatoa taarifa pindi zitakapopatikana.”

Shughuli za uokoaji zilianza kwa haraka, ikiwa ni pamoja na boti kwenye Mto Potomac. Ndege huwa zinapita juu ya mto huo kabla ya kutua kwenye uwanja wa ndege wa Reagan National.

Rais wa Marekani Donald Trump alitoa taarifa akisema amefahamishwa kuhusu tukio hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG