Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Julai 01, 2024 Local time: 21:30

Mtu mmoja auwawa na wengine 200 wajeruhiwa katika maandamano ya nchi nzima Kenya


Anti-finance bill protesters clash with police in Nairobi
Anti-finance bill protesters clash with police in Nairobi

Mtu mmoja aliuwawa na wengine takriban 200 kujeruhiwa kote nchini Kenya katika maandamano ya nchi nzima ya Alhamisi dhidi ya mipango ya serikali ya kuongeza dola bilioni 2.7 kama ushuru wa ziada, muungano wa mashirika ya kutetea haki za binadamu na lile linalofuatilia polisi yalisema.

Polisi walirusha mabomu ya kutoa machozi na maji ya kuwasha kuwatawanya waandamanaji katika mji mkuu Nairobi, mashirika matano ya kutetea haki, pamoja na Amnesty International na Chama cha Madaktari Kenya, yalisema katika taarifa ya pamoja siku ya Alhamisi.

Kuwepo kwa maganda yaliyotumika kulibainisha kulikuwa na matumizi ya risasi walisema, na kuongeza kuwa zaidi ya waandamanaji 100 wamekamatwa kote nchini Kenya.

Mamlaka huru ya Uangalizi wa Polisi (IPOA) ilisema Ijumaa ilikuwa imeorodhesha taarifa ya kifo cha mwanamume mmoja kinachodaiwa kuwa ni matokeo ya kupigwa risasi na polisi na majeraha kadhaa mabaya waliyopata baadhi ya waandamanaji wakiwemo maafisa wa polisi.

Forum

XS
SM
MD
LG