Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Septemba 17, 2024 Local time: 03:19

Mtoto mmoja kati ya watoto wanne anakabiliwa na umaskini wa chakula-UNICEF


Mfano wa mtoto mwenye utapiamlo. Ethiopia, Feb. 23, 2022.
Mfano wa mtoto mwenye utapiamlo. Ethiopia, Feb. 23, 2022.

Mtoto mmoja kati ya watoto wanne walio na umri wa chini ya miaka mitano wanakabiliwa na umaskini mkubwa wa chakula, na kuwaweka katika hatari ya kukabiliwa na utapiamlo unaotishia maisha yao, kulingana na ripoti ya shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia watoto (UNICEF) iliyotolewa Alhamisi.

Asilimia 27 ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano, sawa na watoto milioni 181 wanapata milo isiyozidi miwili kati ya milo minane inayotambuliwa na UNICEF, kiwango ambacho shirika hilo linakiorodhesha kama umaskini mkubwa wa chakula. Kama watoto hawapati lishe muhimu, kuna hatari wanakuwa na uzito dhaifu wa mwili, aina mbaya sana ya utapiamlo.

“Wakati uzito dhaifu wa mwili unakuwa mbaya sana, kuna uwezekano wa mara 12 wa kufariki,” Harriet Torlesse, mmoja wa walioandika ripoti hiyo ameiambia Associated Press.

Zaidi ya theluthi mbili za watoto milioni 181 wanaoishi na umaskini mkali wa chakula wanaishi Asia Kusini na kusini mwa Jangwa la Sahara, huku nchi 20 zikiwa na asilimia 65 ya watoto wanaoishi na umaskini mkali wa chakula.

Umaskini wa chakula huko Gaza umeongezeka sana tangu vita vya Israel dhidi ya Hamas vilipoanza.

Forum

XS
SM
MD
LG