Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Oktoba 08, 2024 Local time: 10:49

Msaada zaidi wa kibinadamu unasubiri kukusanywa Gaza


Misaada ya kibinadamu ya Gaza, Palestina
Misaada ya kibinadamu ya Gaza, Palestina

Msaada wa kibinadamu katika msururu wa lori 1,150 unasubiri kukusanywa katika upande wa Wapalestina wa kivuko cha Kerem Shalom kusini mwa Ukanda wa Gaza, Israel imesema Jumatano, na kuufanya Umoja wa Mataifa kusema inafanya kile iwezacho.

COGAT, wakala wa Wizara ya Ulinzi ya Israel iliyopewa jukumu la kuratibu uwasilishaji wa misaada katika maeneo ya Wapalestina, imesema lori nyingine 50 za misaada pia zinangoja kukusanywa kutoka upande wa Wapalestina wa kivuko cha Erez kaskazini mwa Gaza.

Umoja wa Mataifa umesema unasumbuka kusambaza misaada ndani ya kundi la watu milioni 2.3 huku vita kati ya Israel na wapiganaji wa Palestina Hamas vikiingia mwezi wa 10 huku sheria na utaratibu ukivunjika.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema wanafanya wawezalo kuwafikiwa watu wenye uhitaji walioko Gaza.

Forum

XS
SM
MD
LG