Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 04:55

Msaada wa Australia kwa Vanuatu


Waziri wa ulinzi wa Australia Pat Conroy wakati wa mkutano wa nchi za ASEAN Novemba 16, 2023. PICHA: Reuters
Waziri wa ulinzi wa Australia Pat Conroy wakati wa mkutano wa nchi za ASEAN Novemba 16, 2023. PICHA: Reuters

Australia imeahidi kuendelea kutoa msaada mkubwa kwa nchi za kusini mwa Pacific, katika mkutano kuhusu usalama na Uchumi, uliofanyika leo Alhamisi na Vanuatu wakati wa thathmini ya athari zinazoweza kutokea kufuatia hatua ya rais Donald Trump kupunguza msaada wa Marekani nje ya nchi.

Waziri wa maendeleo ya kimataifa wa Autralia Pat Conroy, ameambia waandishi wa habari katika mji mkuu wa Port Vila nchini Vanuatu kwamba Australia itaendelea kusaidia nchi hiyo.

Conroy, ambaye amefanya mazungumzo na Waziri mkuu wa Vanuatu Jotham Napat, ameahidi msaada kwa bajeti ya Vanuatu, wa kiasi cha dola milioni 3.2, baada ya kutokea tetemeko la ardhi mwezi Desemba lililoharibu nyumba kadhaa na kusababisha vifo vya watu 16.

Conroy amesema kwamba nchi kubwa zinashindana kuwa na ushawishi katika kanda hiyo lakini Australia inajivunia kuwa mshirika mkubwa wa maendeleo, akisisitiza kwamba nchi hiyo ilikuwa inatoa msaada kwa nchi za kanda ya Pacific kabla ya nchi nyingine, ikiwemo Marekani, au China.

Forum

XS
SM
MD
LG