Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 07, 2024 Local time: 15:17

Mpango wa kusitishwa mapigano Gaza wafikia hatua za mwisho


Mazungumzo kuhusu mpango wa kusitisha mapigano katika mzozo wa Gaza yanaonekana kuwa katika hatua za mwisho, na Rais wa Marekani, Joe Biden na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, watajadili mianya iliyosalia leo hii Alhamisi, afisa mkuu wa Marekani amesema Jumatano.

Afisa huyo, akitoa maelezo kwa waandishi wa habari kabla ya mazungumzo yao, amesema vikwazo vilivyosalia vinaweza kutatuliwa na kutakuwa na mikutano zaidi inayolenga kufikia makubaliano kati ya Israel na Hamas ndani ya wiki ijayo.

Wapiganaji wanaoongozwa na Hamas walivamia kusini mwa Israel, 7 Oktoba mwaka jana, na kuua watu 1,200 na kuchukua mateka 250, kwa mujibu wa Israel, na kusababisha vita ambapo zaidi ya watu 38,000 wameuawa Gaza, kwa mujibu wa wizara ya afya ya eneo hilo, ambayo haijatofautisha vifo vya wapiganaji na raia katika hesabu yake.

Forum

XS
SM
MD
LG