Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 20:20

Mashambulizi ya kila upande kati ya Russia na Ukraine


Mwanajeshi wa Ukraine akiwa juu ya kifaru mashariki mwa Donetsk. Dec 13, 2024
Mwanajeshi wa Ukraine akiwa juu ya kifaru mashariki mwa Donetsk. Dec 13, 2024

Maelfu ya watu hawana umeme katika mji wa Odesa, kusini mwa Ukraine, kufuatia mashambulizi ya angani yaliyotekelezwa na Russia.

Gavana wa Odesa Oleh Kiper ameandika ujumbe kwente Telegram kwamba wafanyakazi wanaendelea na juhudi za kurudisha umeme.

Nyumba 49,000 zilikuwa hazina umeme kufikia wakati tunaandaa ripoti hii.

Mashambulizi ya Russia yameendelea leo Alhamisi katika sehemu kadhaa za Ukraine ikiwemo katika eneo la Katikati la Cherkasy ambapo gavana Ihor Taburets amesema mfumo wa ulinzi wa angani umeangusha ndege 14 zisizokuwa na rubani, za Russia.

Taburets amesema kwamba uharibifu umetokea kwenye biashara na kukatiza nguvu za umeme lakini hakuna vifo vimeripotiwa.

Gavana wa Mykolaiv Vitaliy Kim, ameripoti kwamba jeshi limeangusha ndege isiyokuwa na rubani iliyokuwa inapaa eneo hilo.

Wizara ya ulinzi ya Russia imesema imeharibu ndege nne zisizokuwa na rubani za Ukraine, usiku wa kuamkia leo, ikiwemo katika eneo linalokaliwa na Russia la Crimea na Bryansk.

Forum

XS
SM
MD
LG