Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Oktoba 05, 2024 Local time: 14:18

Mashambulizi ya anga ya Russia yaharibu makumbusho Ukraine


Ndege zisizo na rubani za Russia, Jumatatu zimeshambulia chuo kikuu na makumbusho maarufu ya watetezi wa utaifa wa Ukraine, wa karne ya 20, lakini wakazi wameapa kufanya matengenezo ya sehemu zilizo haribika.

Kwanza yaliharibu madirisha, na sehemu kubwa ya paa la chuo kikuu cha taifa cha Agrarian kilichopo nje kidogo ya mji wa Lviv, ambapo Stepan Bandera, shujaa wa Ukraine ambaye Kremlin inamchukulia kama mnyama alisoma.

Mashambulizi hayo yamefanyika katika kipindi ambacho ni maadhimisho ya miaka 115 ya kuzaliwa kwa Bandera.

Shambulizi la pili liliharibu makumbusho ambayo yametengwa kwa ajili ya Roman Shukhevych.

Wote wawili hao ni vielelezo muhimu kwa kudai utaifa wao kutoka kwa utawala wa Kisovieti, ambao ulikuwa ukihusishwa na kundi la wanamgambo wa Ukraine, UPA ambao ulipambana na vikosi vya Kisovoeti, katika vita vya pili vya dunia.

Forum

XS
SM
MD
LG