Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 03, 2025 Local time: 00:04

Marekani yatoa onyo kwa Panama kuhusu matumizi ya mfereji wa Panama


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio akihutubia familia na wafanyakazi kwenye ubaozi wa Marekani mjini Panama City, Panama, Jumapili, February 2, 2025.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio akihutubia familia na wafanyakazi kwenye ubaozi wa Marekani mjini Panama City, Panama, Jumapili, February 2, 2025.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio Jumapili ameambia viongozi wa Panama kwamba China ina ushawishi hatari kwenye mrefeji wa Panama, na kwamba iwapo hilo halitabadishwa, basi huenda Marekani ikalazimika kuchukua hatua muhimu za kulinda haki yake ya kutumia mfereji huo.

Rubio ameambia rais wa Panama Jose Raul Mulino na waziri wa mambo ya kigeni Javier Martinez Acha, wakiwa kwenye mji wa Panama City, kwamba Rais wa Marekani Donald Trump amefanya maamuzi ya kwanza kwamba msimamo wa sasa, ushawishi na udhibiti wa Chama cha Kikomumisti cha China kwenye mfereji wa Panamana ni tishio kwenye operesheni zake, wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema.

Hata hivyo taarifa hiyo haikufafanua ni ushawishi wa aina gani ambao Marekani inadai kuwa nao kwenye mfereji huo wenye urefu wa kilomita 82 kati ya bahari za Atlantic na Pacific, hatua inazopanga kuchukua, wala majibu ya Rais wa Panama kutokana na taarifa ya Rubio. Rais huyo katika siku za karibuni amelalamikia ukosoaji kutoka Marekani hukusu namna mfereji huo unavyoendeshwa, ukiwa na umuhimu mkubwa kwenye biashara za kimataifa.

Hata hivyo alisema kuwa hakutakiwa na majadiliano yoyote na Marekani kuhusu umiliki wa mfereji huo, huku baadhi ya wakazi wa Panama wakifanya maandamano kupinga mpango wa Marekani.

Forum

XS
SM
MD
LG