Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 05:48

Mapigano yatokea baina ya vikosi vya serekali ya Somalia na Al Shabab


Mapigano makali yameripotiwa katikati mwa Somalia baada ya wanamgambo wa Al Shabab kuvamia kambi ya jeshi la serekali katika mji wa Masagaway, Jumanne ikiwa ni shambulizi la pili katika siku kadhaa.

Vyanzo vya usalama ambavyo vinafuatilia hali hiyo vinasema mapigano yameshirikisha vikosi vya serekali na Al Shabab baada ya shambulizi la wanamgambo hao.

Kwa mujibu wa afisa mmoja wa usalama aliyehusika katika makabiliano na Al Shabab, anasema wanamgambo hao walivamia kambi ya kijeshi alfajiri.

Kambi hiyo hutumiwa na vikosi vinavyopewa mafunzo na Eritrea, na wapiganaji wa huko.

Amesema wanamgambo walifanikiwa kuingia kambini na kuondoa magari matatu.

Baada ya wanamgambo kutoka katika mji, oparesheni kutoka mji wa el-Dheer ulioko kaskazini mwa Masagaway ilianza kwa kuwavamia wanamgambo wa Al Shabab na mapambano makali kuanza.

Forum

XS
SM
MD
LG