Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Septemba 13, 2024 Local time: 08:22

Mapigano yaendelea Ukanda wa  Gaza wakati Marekani, Qatar na Misri wanatafuta sitisho la mapigano


Picha hii iliyotolewa na Ofisi ya Rais wa Misri inamuonyesha Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi (katikati) akikutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken (Kushoto) na ujumbe wake huko Alamein kaskazini mwa Misri Agosti 20, 2024.
Picha hii iliyotolewa na Ofisi ya Rais wa Misri inamuonyesha Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi (katikati) akikutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken (Kushoto) na ujumbe wake huko Alamein kaskazini mwa Misri Agosti 20, 2024.

Mapigano yaliendelea katikati mwa Ukanda wa  Gaza siku ya Ijumaa, hata wakati Marekani, Qatar na Misri ziliposonga mbele kujaribu kufanikisha  makubaliano ya kusitisha mapigano.

Silaha nzito na bunduki za rashasha zilisikika zikifyatuliwa alfajiri karibu na mashariki mwa Deir al-Balah katika video iliyochukuliwa na The Associated Press, huku mitaa ikiwa haina watu.

Katika mji wa kusini wa Khan Younis, watu wanne waliuawa katika shambulizi la mapema la Israel dhidi ya gari lao, alisema msemaji wa Ulinzi wa Raia wa Palestina Mahmoud Bassal.

Bassal aliripoti Alhamisi usiku kwamba watu 24 waliuawa siku moja kabla katika mashambulizi kadhaa kote Ukanda wa Gaza na jeshi la Israeli, pamoja na Gaza City upande wa kaskazini na Khan Younis upande wa Kusini.

Alisema mashambulizi hayo pia yalisababisha majeruhi wengi lakini hakueleza ni wangapi.

Forum

XS
SM
MD
LG