Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 21:37

Mapigano ya kudhibiti mji wa Goma yanaendelea-Afisa wa UN


Watu waliokimbia makazi yao kutokana na mapigano ya M23 wakielekea katikati mwa Goma, Januari 26, 2025. Picha ya AP
Watu waliokimbia makazi yao kutokana na mapigano ya M23 wakielekea katikati mwa Goma, Januari 26, 2025. Picha ya AP

Afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Jumatatu alisema kwamba mapigano kati ya waasi wa M23 na jeshi la Congo katika mji mkuu muhimu wa mashariki mwa nchi yalikuwa “hayajamalizika”, licha ya waasi hao kudai kwamba waliuteka mji wa Goma.

“Mapigano bado yanaendelea,” alisema Bruno Lemarquis, mwakilishi wa Umoja wa Mataifa nchini DRC.

“Ni hali ya kutatanisha. Ni hali hatari sana.”

Aliwambia waandishi wa habari kupitia mahojiano ya video akiwa katika mji mkuu wa DRC, Kinshasa kwamba “ Mapigano makali yamekuwa yakiendelea katika mitaa yote” ya Goma huko Kivu Kaskazini.

Lemarquis alisema kumekuwa na tatizo kubwa la maji, umeme, intaneti na huduma ya simu. Maghala ya misaada ya kibinadamu yameporwa.

“Kwa niaba ya jumuia ya mashirika ya misaada ya kibanadamu, natoa wito kwa pande zote kukubaliana juu ya sitisho la muda la mapigano katika maeneo yanayoathirika zaidi na kutoa njia salama kuhakikisha shughuli za kutoa misaada zinaanza tena. Na muhimu zaidi, kurahisisha pia njia salama ili kuwaondoa watu waliojeruhiwa na raia waliobanwa katika maeneo ya mapigano,” Lemarquis aliongeza.

Umoja wa Mataifa Jumapili ulitangaza msaada wa dola milioni 17 kutoka kwenye mfuko wake wa dharura kwa ajili ya mahitaji muhimu ya kibinadamu nchini DRC.

Hayo yakiarifiwa, mapigano ya wapiganaji wa M23 na jeshi la Congo mjini Goma, yameua takriban watu 17 na kujeruhi wengine 367, kulingana na takwimu za hospitali kadhaa ambazo zimeonwa na shirika la habari la AFP.

Forum

XS
SM
MD
LG