Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 14, 2025 Local time: 03:53

Mahakama ya katiba Korea Kusini inapitia upya mashtaka ya Rais Yoon Suk Yeol


Rais wa Korea Kusini Yoon Suk Yeol katika picha ya hivi karibuni wakati alipokuwa akilihutubia taifa.
Rais wa Korea Kusini Yoon Suk Yeol katika picha ya hivi karibuni wakati alipokuwa akilihutubia taifa.

Mahakama itafanya kikao cha kwanza cha umma Disemba 27 baada ya majaji sita wa mahakama kukutana.

Mahakama ya Katiba ya Korea Kusini leo Jumatatu ilianza kupitia upya mashtaka ya kutaka kumuondoa madarakani Rais Yoon Suk Yeol kwa tangazo lake la sheria ya kijeshi la Disemba 3 na kuanza mchakato wa kuamua kama ataondolewa madarakani, wakati wachunguzi wanapanga kumhoji wiki hii juu ya mashtaka ya uhalifu.

Mahakama hiyo itafanya kikao cha kwanza cha umma hapo Disemba 27, msemaji Lee Jean aliwaambia waandishi wa habari baada ya majaji sita wa mahakama hiyo kukutana ili kujadili mipango ya kutathmini mashtaka ya kumuondoa madarakani, na bunge linalodhibitiwa na upinzani siku ya Jumamosi.

Mahakama hiyo ina hadi miezi sita kuamua iwapo itamuondoa Yoon madarakani au kumrejesha. Usikilizaji wa kwanza utakuwa “maandalizi” ya kuthibitisha masuala makuu ya kisheria ya kesi na ratiba kati ya mambo mengine, Lee alisema.

Forum

XS
SM
MD
LG