Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Julai 01, 2024 Local time: 23:05

Mahakama kuu Namibia yatangaza kuwa kinyume cha katiba kwa sheria mbili ambazo ziliharamisha mapenzi ya jinsia moja


Watu wameshikilia mabango kuunga mkono haki za LGBTQ nje ya mahakama kuu ambayo ilifanya uamuzi wa kihistoria kupendelea jumuiya za wapenzi wa jinsia moja huko Windhoek, Namibia, Juni 21, 2024
Watu wameshikilia mabango kuunga mkono haki za LGBTQ nje ya mahakama kuu ambayo ilifanya uamuzi wa kihistoria kupendelea jumuiya za wapenzi wa jinsia moja huko Windhoek, Namibia, Juni 21, 2024

Mahakama kuu nchini Namibia siku ya Ijumaa ilitangaza kuwa kinyume cha katiba kwa sheria mbili za enzi za ukoloni ambazo ziliharamisha mapenzi ya jinsia moja kati ya wanaume, katika ushindi wa kihistoria kwa watu wa jumuiya ya mapenzi ya jinisa moja - LGBTQ katika taifa hilo la kusini mwa Afrika.

Kesi hiyo iliwasilishwa na mwanaharakati wa Namibia Friedel Dausab kwa msaada wa shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake makuu nchini Uingereza Human Dignity Trust.

Dausab aliliambia shirika la habari la Reuters baada ya uamuzi huo wa mahakama kuwa alikuwa na furaha. Ni siku nzuri kwa Namibia alisema. Haitakuwa kosa tena kupenda.

Wanaharakati wa haki wanasema kwamba wakati hukumu chini ya sheria juu ya ulawiti na makosa yasiyo ya asili ya ngono ilikuwa nadra sana, wameendeleza ubaguzi dhidi ya jamii ya watu wa mapeni ya jinsia moja -LGBTQ na kuwafanya mashoga kuishi kwa hofu ya kukamatwa.

Forum

XS
SM
MD
LG