Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Oktoba 10, 2024 Local time: 06:29

Korea Kaskazini yasema itaendelea kuwa na nyuklia kukabiliana na Marekani


Korea Kaskazini, Jumamosi imeapa kuendeleza uwezo wake wa nyuklia, ikijibu ripoti kwamba Marekani imepitia upya mipango yake ya kimkakati ya nyuklia.

Shirika la habari la serikali ya Korea Kaskazini, KCNA limeripoti kwamba, “nchi itaendelea kuboresha mkakati wake wa uimara katika kila nyanja, na kuondoa aina yoyote ya changamoto za kiusalama ambazo zitakuwa ni matokeo ya mpango uliopitiwa upya wa Washington.”

Gazeti la New York Times wiki hii liliripoti kwamba mpango wa Marekani uliopitishwa na Rais Joe Biden, mwezi Machi, ulikuwa kwa ajili ya kuandaa uwezekano wa uratibu wa kukabiliana na Russia, China, na Korea Kaskazini.

Mpango huo ambao ni siri kubwa kwa mara ya kwanza unaeleza mpango wa kimkakati wa Washington, kujikita kwa kukabiliana na upanuzi mkubwa wa program ya silaha za nyuklia za China, kwa mujibu wa gazeti la The New York Times.

Forum

XS
SM
MD
LG