Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 12, 2024 Local time: 00:09

Kesi zaidi ya elfu 18 zinazoshukiwa za ugonjwa wa Mpox zaripotiwa barani Afrika tangu mwanzoni mwa mwaka


Mhudumu wa afya akibeba trei katika kituo cha matibabu cha Mpox katika Hospitali Kuu ya Rufaa ya Nyiragongo, kaskazini mwa Goma Agosti 17, 2024.
Mhudumu wa afya akibeba trei katika kituo cha matibabu cha Mpox katika Hospitali Kuu ya Rufaa ya Nyiragongo, kaskazini mwa Goma Agosti 17, 2024.

Jumla ya kesi 18,737 zinazoshukiwa au kuthibitishwa za ugonjwa wa mpox ziliripotiwa barani Afrika tangu mwanzoni mwa mwaka, ikiwa ni pamoja na kesi 1,200 katika wiki moja pekee, shirika la afya la Umoja wa Afrika lilisema leo Jumamosi.

Idadi hiyo inachangia aina tatu za virusi hivyo, moja kati ya hizo ni Clade 1b mpya ambayo ni hatari zaidi na inayoweza kuambukizwa zaidi ambayo ilisababisha Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) siku ya Jumatano kutangaza dharura ya kiafya ya kimataifa tahadhari ya juu zaidi ya shirika hilo.

Hadi sasa, kesi 3,101 zilizothibitishwa na 15,636 zinazoshukiwa zimeripotiwa kutoka nchi 12 wanachama wa Umoja wa Afrika, na kusababisha vifo 541 kiwango cha vifo cha asilimia 2.89, Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) vilisema katika taarifa.

Forum

XS
SM
MD
LG