Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Septemba 29, 2024 Local time: 04:26

Kenya yasitisha mradi wa fedha za kidijitali 'Worldcoin crypto'


Aina tofauti ya fedha za kidijitali
Aina tofauti ya fedha za kidijitali

Kenya Jumatano ilisitisha mradi wa fedha za kidijitali unaojulikana kama Worldcoin crypto, ambao unatumia ukaguzi wa macho ya mtu ili kuthibitisha utambulisho wa mtumiaji, ikitaja hofu ya kulinda taarifa za siri.

Mfumo wa Worldcoin ambao ulianzishwa na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya OpenAl, Sam Altman, ulianza kufanya kazi mwezi Juni nchini Ujerumani na unawapa watumiaji utambulisho wa kibinafsi wa kidijitali, baada ya kukaguliwa sehemu ya macho yao iitwayo Iris.

Mradi huo kulingana na waanzilishi wake, unalenga kutatua moja ya changamoto kuu zinazokabili sekta ya crypto ambayo kwa kiasi kikubwa inatumia majina bandia ili kufanya kazi, na kuiweka katika hatari ya kutumiwa na matapeli.

Watumiaji waliojiandikisha katika mradi huo nchini Kenya walipewa tokeni 25 za bure za Worldcoin zenye thamani ya shilingi 7,000, na kuwavutia maelfu ya watu kwenye vituo vingi vya kujisajili katika mji mkuu Nairobi.

Waziri wa mambo ya ndani Kithure Kindiki alisema mamlaka “zilitiwa wasiwasi” na mradi huo na zimeanzisha uchunguzi ili kubaini “usalama na ulinzi wa taarifa za siri zinazokaguliwa, na jinsi wakaguzi wanakusudia kutumia taarifa hizo”.

Forum

XS
SM
MD
LG