Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 19, 2024 Local time: 01:45

Kenya Airways imetangaza kupata faida yake ya kwanza ya nusu mwaka


Shirika la ndege la Kenya-Kenya Airways katika uwanja wa ndage wa kimataifa wa Jomo Kenyatta Nairobi. Aug. 1, 2020.
Shirika la ndege la Kenya-Kenya Airways katika uwanja wa ndage wa kimataifa wa Jomo Kenyatta Nairobi. Aug. 1, 2020.

Shirika hilo lilipata faida baada ya kukatwa kodi ya shilingi milioni 513 kuanzia Januari hadi Juni

Shirika la ndege la Kenya limetangaza Jumatatu faida yake ya kwanza ya nusu mwaka katika zaidi ya miaka 10, ilitokana na kuongezeka kwa idadi ya abiria, na ilisema ilikuwa ikitumaini itaweza kufunga rekodi hata kwa mwaka mzima.

Shirika hilo la ndege lilipata faida baada ya kukatwa kodi ya shilingi milioni 513 kuanzia Januari hadi Juni, na kubadilisha hasara ya shilingi bilioni 21.7 katika nusu ya kwanza ya 2023.

Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo Allan Kilavuka, aliwaambia waandishi wa habari kwamba kampuni ilikuwa ikikamilisha mashauriano yanayohusu usawa wa kimkakati kwa mwekezaji, bila kutoa maelezo.

Moja ya mashirika matatu makubwa ya ndege barani Afrika, Kenya Airways lilifilisika mwaka 2018 baada ya upanuzi wa shirika hilo kuingia katika deni la mamilioni ya dola.

Forum

XS
SM
MD
LG