Kulingana na vyanzo vya habari za uslama vimeambia VOA kwamba wafungwa waliokuwa wapiganaji, katika gereza kuu la Mogadishu, wakitumia bastola na guruneti, walishambulia walinzi wa gereza hilo.
Wafungwa hao wamefytua risasi dhidi ya walinzi na kulipua gruneti, kabla ya mashambuliano ya risasi kuanza.
Inaaminika kwamba silaha hizo ziliingizwa gerezani kwa njia ya magendo.
Maafisa wa usalama wamesema kwamba wamedhibithi hali katika gereza hilo na msemaji wa huduma ya magereza Abdiqani Mohamed Khalaf, ameambia waandishi wa habari kwamba walinzi watatu wa magereza wameuawa katika tukio hilo na wengine watatu kujeruhiwa.
Forum