Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Septemba 23, 2024 Local time: 20:19

Israel yashambulia kwa ndege za kivita Lebanon


Moshi uliotanda katika shambulizi la ndege la Israel, Lebanon
Moshi uliotanda katika shambulizi la ndege la Israel, Lebanon

Ndege za Israel zimefanya shambulizi la silaha za kimakati za Hezbulah zilizofichwa kwenye nyumba katika bonde la Bekaa nchini Lebanon, msemaji wa jeshi la Israel Daniel Hagari amesema leo akitoa wito kwa raia kuondoka mara moja.

Israel ilishambulia mamia ya malengo ya Hezbolah Jumatatu kwa mashambulizi ya anga ambayo maafisa wa afya wa Lebanon wanasema yameuwa takriban watu zaidi ya 270 na kufanya kuwa shambulizi lenye mauaji makubwa nchini humo katika karibu mwaka mmoja wa mzozo.

Baada ya mapambano makali ya mpakani tangu mzozo ulipozuka , Israel imewaonya watu kuhama katika maeneo ambayo wamesema kundi lenye silaha lilikuwa linahifadhi silaha.

Karibu mwaka mmoja wa vita dhidi ya Hamas huko Gaza katika mpaka wake wa kusini , Israel inahamisha lengo lake katika mpaka wa kaskazini, ambako kundi la Hezbolah linaloungwa mkono na Iran limekuwa likifyatua roketi nfani ya ISRAEL kumuunga mkono mshirika wake Hamas.

Forum

XS
SM
MD
LG