Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 21:02

Israel na Hamas wabadilishana mateka na wafungwa wengine


Wanamgambo wa Hamas na Islamic Jihad wakilinda eneo ambako kumefanyika ubadilishanaji wa mateka, Januari 30, 2025. Picha ya AP
Wanamgambo wa Hamas na Islamic Jihad wakilinda eneo ambako kumefanyika ubadilishanaji wa mateka, Januari 30, 2025. Picha ya AP

Jeshi la Israel limesema mateka wanane, wakiwemo Waisraeli watatu na raia watano wa Thailand, waliachiliwa Alhamisi huku Israel na Hamas wakifanya ubadilishanaji wa tatu wa mateka na wafungwa chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano ya zaidi ya miezi 15 huko Gaza.

Mwanajeshi mwanamke wa Israel Agam Berger aliachiliwa na kukabidhiwa Shirika la Msalaba Mwekundu katika kambi ya wakimbizi ya Jabaliya kaskazini mwa Gaza, na baadaye alikwenda Israel, ambako aliungana tena na wazazi wake.

Saa chache baadaye, msafara wa Shirika la Msalaba Mwekundu ulipita kwenye barabara yenye msongamano iliyojaa umati wa watu katika mji wa kusini mwa Gaza wa Khan Younis ili kuwakabidhi Waisraeli wengine wawili na raia wa Thailand kwa jeshi la Israel.

Jeshi la Israel lilisema Waisraeli hao wataungana na familia zao, huku maafisa wa serikali ya Thailand wakitarajiwa kukutana na raia wao.

Baadaye mchana, kama sehemu ya makubaliano ya kusitisha mapigano, Israel iliwaachilia Wafungwa 110 wa Kipalestina, wakiwemo 32 waliokuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela kutokana na mashambulizi mabaya dhidi ya Waisraeli.

Forum

XS
SM
MD
LG