Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Septemba 09, 2024 Local time: 09:14

Israel imethibitisha kifo cha kamanda wa Hamas aliyepanga shambulizi la Oktoba 7


Msemaji wa jeshi la Israel Admiral Daniel Hagari
Msemaji wa jeshi la Israel Admiral Daniel Hagari

Israel Alhamisi ilisema ilimuua kiongozi wa kijeshi wa Hamas Muhammad Dief, anayemaanika kuwa ndiye alipanga shambulizi la Hamas la Oktoba 7 dhidi ya Israel, katika mji wa kusini mwa Gaza wa Khan Younis katikati mwa mwezi Julai.

Waziri wa ulinzi Yoav Gallant alimtaja Deif kuwa “Osama bin Laden wa Gaza”, akimaanisha Bin Laden aliyepanga shambulizi la 2001 la kundi la kigaidi la al-Qaeda nchini Marekani ambalo liliua karibu watu 3,000.

Gallant alisema kuuawa kwa Deif tarehe 13 Julai “ ni hatua kubwa katika mchakato wa kulisambaratisha kundi la Hamas kama jeshi na mamlaka inayotawala huko Gaza, na katika kufikia malengo ya vita hivi.”

Jeshi la Israel lilisema katika taarifa kwamba lilithibitisha kuwa Deif alikufa kulingana na tathmini ya kijasusi lakini halikutoa maelezo zaidi.

Israel ilikuwa imemlenga katika shambulizi lililoua watu 90, lakini hatma ya Deif haikujulikana.

Hamas haijathibitisha au kukanusha kifo chake.

Forum

XS
SM
MD
LG