Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 15:07

Israel imeshambulia Hezbollah


Jeshi la Israel likishika doria kusini mwa Lebanon.
Jeshi la Israel likishika doria kusini mwa Lebanon.

Jeshi la Israel limesema limepiga ngome za kundi la wanamgambo wa Hezbollah usiku wa kuamkia leo katika bonde la Bekaa, kwenye mpaka wa Syria na Lebanon.

Israel imesema miongoni mwa sehemu zilizopigwa ni kiwanda cha siri kinachotumika kutengeneza silaha na sehemu nyingine inayohusishwa na uingizaji kwa magendo silaha ndani ya Lebanon.

Israel ilisema jana alhamisi kwamba walinasa ndege isiyokuwa na rubani iliyokuwa inafanya ujasusi kwa msingi kwamba ilikuwa inavunja makubaliano ya kusitisha vita kati ya Israel na Lebanon.

Hezbollah na Israel walikubaliana kusitisha vita mwishoni mwa mwezi Novemba na kumaliza mapigano mabaya yaliyoanzia Gaza mwaka 2023.

Marekani ilithibitisha mnamo Jumapili kwamba makubaliano hayo yanayojumulisha siku 60 za wanajeshi wa Israel kuondoka Lebanon, yataendelea kutumika hadi Februari 18.

Israel imetekeleza mashambulizi kadhaa ndani ya Lebanon tangu makubaliano yalipofikiwa, na kuua na kuwajeruhi zaidi ya watu 100.

Forum

XS
SM
MD
LG