Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Agosti 22, 2024 Local time: 20:32

Hali ya taharuki yaendelea kutanda kati ya Korea Kaskazini na Kusini kutokana na puto na vijikaratasi vyenye chuki


Dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Yo Jong.
Dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Yo Jong.

Dada mwenye nguvu wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, Kim Yo Jong, Jumapili ameapa kujibu kampeni mpya ya Korea Kusini ya kuandika mabango dhidi ya Korea Kaskazini, ikiashiria kuwa taifa hilo huenda likaanza tena kurusha puto zenye takataka ndani ya Korea Kusini.

Tangu mwishoni mwa Mei, Korea Kaskazini imerusha puto nyingi zikiwa zimebeba taka za aina tofauti pamoja na mbolea kuelekea Korea Kusini, hilo likifanyika nyakati za usiku, dada yake Kim akisema kuwa yalikuwa majibu dhidi ya wanaharakati wa Korea Kaskazini kurusha vijikaratasi vyenye maneno ya kisiasa dhidi ya Kaskazini.

Kufikia sasa hakuna taka zenye sumu zilizorushwa. Korea Kusini ilijibu kwa kusitisha makubaliano ya 2018 ya kupunguza taharuki na Korea Kaskazini, wakati ikirejea tena mazoezi ya silaha za moto kwenye mpaka. Kupitia taarifa iliotolewa kupitia vyombo vya habari vya serikali.

Kim Yo Jong amesema kuwa majikaratasi yenye matusi kutoka Korea Kusini yamepatikana tena kwenye mpaka na kwenye baadhi ya maeneo ndani ya Korea Kaskazini. Ameongeza kusema kuwa licha ya maonyo kutoka Kaskazini, Korea Kusini inaendelea na mchezo huo mbaya.

Forum

XS
SM
MD
LG