Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Juni 29, 2024 Local time: 19:42

Gutteres ataka wafanyakazi wa UM kuachiliwa Yemen


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, Jumanne ametoa mwito wa kuachiliwa mara moja kwa wafanyikazi wote wanaoshikiliwa Yemen na maafisa wa serikali ya Kihouthi.

Waasi wanaoungwa mkono na Iran, Jumatatu walitangaza kuwakamata wafanyakazi 13 wa Umoja wa Mataifa wakidai kuwa mwajiri wao anahusishwa na idara ya ujajusi ya Marekani, CIA na kwamba wamekuwa wakiendesha operesheni za kijasusi nchini humo kwa miaka mingi.

Wafanyakazi wengine wanne wa Umoja wa Mataifa wamezuiliwa nchini humo toka walipokamatwa mwaka 2021 na 2023.

Hawajana mawasiliano na mwajiri au familia zao. Akikutana na mjumbe maalumu kwa Yemen, Hans Grundberg, Jumanne, Katibu Mkuu Guterres, amesema anapinga madai ya Wahodhi, huku akiwa na wasiwasi mkubwa wa hali za wafanyakazi wanaoshikiliwa.

Forum

XS
SM
MD
LG