Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 07, 2024 Local time: 09:57

Fatah na Hamas zadai kupatana kuunda serekali ya kitaifa Palestina


Mahmoud al-Aloul, wa Fatah, Waziri wa mambo ya nje wa China, Wang Yi, na Mussa Abu Marzuk, wa Hamas, wakiwa mjini Beijing, Julai 23, 2024.
Mahmoud al-Aloul, wa Fatah, Waziri wa mambo ya nje wa China, Wang Yi, na Mussa Abu Marzuk, wa Hamas, wakiwa mjini Beijing, Julai 23, 2024.

Pande hasimu za Palestina, Fatah na Hamas zimetia saini azimio jijini Beijing la kumaliza mifarakano ya miaka mingi na kuungana kuunda serikali ya umoja wa kitaifa, China imetangaza Jumanne.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Mao Ning, amesema wawakilishi wakuu wa makundi 14 ya Palestina walifanya mazungumzo ya maridhiano mjini Beijing kuanzia Julai 21 hadi 23, na kutia saini tamko la Beijing juu ya kumaliza mgawanyiko na kuimarisha umoja wa kitaifa wa Palestina.

Mjini Washington, maafisa wa Marekani wanasema bado hawajapitia makubaliano hayo.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Matthew Miller, Jumanne alikiri kwamba Marekani imeitangaza Hamas kuwa taasisi ya kigaidi na Washington haioni nafasi yoyote kwa Hamas katika utawala wa baada ya vita wa Gaza.

Forum

XS
SM
MD
LG